Chagua
samaki wazazi wazuri kulingana na umbile lao kama rangi, ukubwa, afya na sura
zao. Samaki hawa watengwe na wale wasio na sifa hizo na wasiruhusiwe kuzaliana
nao. Mfugaji anaweza kununua wazazi hawa kutoka katika chanzo kinachofahamika
kuwa kina samaki bora.
Dhibiti
ubora wa samaki hawa wazazi kwa kutoruhusu miingiliano na samaki wenye ubora
hafifu. Chuja vema maji yanayoingia bwawa. Ikiwezekana, tumia samaki wenye
ukubwa wa zaidi ya gramu 100. Hii itakuwezesha kutenganisha wazazi kutoka kwa
vifaranga kila baada ya kuzaliwa (reproduction cycle).
Endelea
kuwatumia wazazi hawa kila unapohitaji vifaranga kutegemeana na jinsi
wanavyoendelea kuzaa vifaranga bora. Pamoja na ubora wa wazazi hawa, kuna
umuhimu wa kuchagua na kuwaondoa vifaranga wasio kuwa na ubora unaohitajika au
ambao ubora wao unatiliwa mashaka (culling).
Ni
muhimu mfugaji afahamu uzuri wa kutumia vifaranga bora. Kausha bwawa kabisa
angalau mara moja kila baada ya miezi sita hadi nane ili kuondokana na samaki
wasio na ubora unao hitajika, kuua maadui wa samaki na kuondokana na hali ya
kuwa na samaki wengi kwenye bwawa zaidi ya kiwango kinachotakiwa na pia hali ya
samaki kuzaliana kinasaba “inbreeding”.
“Culling na grading” ni muhimu kuanza baada ya siku 30 hadi 45 baada ya
samaki wakubwa kuwa wamewekwa kwenye bwawa na hufanyika kwa kutumia kawavu kadogo
ambacho kina matundu madogo.
Endelea
kufanya kazi hii kila baada ya wiki mbili hadi nne.
Urutubishaji wa bwawa na ulishaji wa samaki
Mfugaji
anashauriwa kuweka mbaleo ya asili kama Mbuji
na samadi kwenye maji kabla ya kupandikiza samaki. Hii ni muhimu kwani
samaki watakaopandikizwa, watahitaji chakula siku hiyo hiyo na chakula chao cha
awali huwa ni vijimea na vijidudu vilivyomo ndani ya maji. Vyote hivi huwepo
kwa wingi kwenye maji yenye rutuba.
Iwapo
maji yatakuwa yamerutubishwa vema, chakula cha ziada huhitajika kwa kiasi
kidogo sana, kama (2-3%) ya uzito wa samaki husika kwa siku. Ni vema samaki
wakalishwa angalau mara mbili, kiasi kidogo asubuhi ya kati ya saa tatu na nne
na jioni kati ya saa 10 na 11. Pia ni vema kama eneo la kulishia ikawa ni
sehemu moja ili kuwazoesha samaki kuja eneo hilo muda wa kulisha na kuwawezesha
kula sehemu kubwa ya chakula watakachopewa.