Jumatano, 1 Agosti 2018

HATUA KWA HATUA NAMNA YA KUANZISHA SHAMBA LA UFUGAJI SAMAKI KWENYE VIZIMBA

Habari za Kazi Wasomaji wa Ukurasa huu.

Ni wakati Mwingine tena tunakutana na kushirikishana katika masuala ya Uzalishaji wa Samaki na Mazao yake. Baada ya Kuona Ongezeko la Maombi ya Uanzishwaji wa Ufugaji wa Samaki kwenye Vizimba, nimeona ni vyema nikawaletea andiko hili kama Kichwa cha habari hapo juu kinavyo someka. Hii imechangiwa na baadhi ya Wawekezaji hasa wa ndani kutokuwa na uelewa wa kutosha jinsi au hatua za kufuata ili waweze kuwekeza katika Tasnia ya Ukuzaji Viumbe Kwenye Maji kwa njia ya Vizimba.

Kwa ufupi ufugaji huu wa Samaki Kwanjia ya Vizimba ni teknolojia inayotumia Maji Machache, kuzalisha Samaki Wengi katika Eneo dogo lililo zungukwa na Nyavu Ndani ya Maji. Fungua link ifuatayo hapa chini kupata kujua mengi zaidi na kuruhusiwa kwa Ufugaji wa Samaki kwa njia ya Vizimba Tanzania. Ufugaji wa Samaki Kwa Njia ya Vizimba-Tanzania




Hivyo, Ili kuweza kupata Kibali cha kufanya Ufugaji wa Samaki kwa Njia ya Vizimba kama yalivyoandaliwa na Idara ya Ukuzaji wa Viumbe kwenye Maji-Wizara ya Mifugo na Uvuvi.


Zifuatazo ni hatua zinazopendekezwa kufyatwa ili mwekezaji aweze kupata kibali cha ufugaji samaki kwenye vizimba.

  1.  Mwekezaji au Mkulima ataanza kwa kutembelea mamlaka za uvuvi zilizopo kwenye eneo ambalo ufugaji kwa njia ya vizimba unatarajiwa kuwekezwa ili kupata taarifa ya mahitaji na matarajio ya uwekezaji,
  2. Katika hatua hii, mkulima au mwekezaji anatakiwa kuthibitisha uraia wake, kwa kuwasilisha vitambulisho au nyaraka zitakazothibitisha uraia wake,
  3. Kwa nyongeza, raia wa kigeni wanatakiwa kuwasilisha leseni ya uwekezaji zinazotolewa na mamlaka ya uwekezaji, 
  4. Taarifa ya  Ufanisi wa Eneo inayotolewa na Mamlaka husika kutoka eneo la Uwekezaji
  5. Mwekezaji au Mkulima anayetaka kuanzisha Ufugaji wa samaki kwenye Vizimba atatakiwa kuwasilisha katika Mamlaka husika kwa ajili ya kupitishwa, Mpango wa uanzishwaji ikiwa ni pamoja na Maelezo ya Makadirio na uendeshaji wa shamba kulingana na yaliyotajwa kwenye Mwongozo wa Ufugaji Samaki kwenye Vizimba pamoja na habari zifuatazo; Majina ya Mameneja na Anwani za Taasisi na, aina ya teknolojia ya Ukuzaji Viumbe kwenye Maji itakayo tumiwa,
  6. Mpango wa kudhibiti majitaka ikiwa ni pamoja na hatua za matibabu ya majitaka ya shamba katika mazingira na hatua za uchunguzi ili kuepuka kutoroka kwa samaki wanaofugwa,
  7. Kibali cha Matumizi ya Maji endapo matumizi yatazidi 400m3 kwa siku,
  8. Ushahidi wa kushirikishwa jamii na mashirikiano ya kijamii jirani na eneo la uwekezaji 
  9. Hati ya Usajili wa biashara “Certificate of incorporation” and “Registration of business
  10. Leseni ya Biashara,
  11. Ushahidi wa Chakula cha Samaki kinapopatikana kutoka kwa chanzo kilichothibitishwa,
  12. Ushahidi wa Vifaranga vya Samaki vinapopatikana kutoka kwa chanzo kilichothibitishwa,
Ikiwa mahitaji haya yatatimizwa, mwekezaji/mkulima atapewa kibali cha muda wa miaka miwili ya kuanzisha na kufanya shughuli ya ufugaji samaki kwenye Vizimba. Katika hatua hii, Mkulima/Mwekezaji anaweza kuanzisha shamba la samaki kwenye eneo lililokubaliwa. Waombaji wanaoidhinishwa wanapewa idhini na vyeti, na huongezwa kwenye orodha ya vyeti vya kuthibitishwa, kuzalisha na kuuza mazao ya ufugaji wa samaki katika soko la ndani na / au nje ikiwa yanakidhi mahitaji ya Soko la kuuza Nje.
Maombi mapya yatafanyika mara kwa mara wakati wowote kama mabadiliko makubwa yamefanywa kwa Mpango uliothibitishwa awali. Wakati wa uendeshaji na uanzishwaji, wakulima au wawekezaji wanatarajiwa kuzingatia Sera zote zinazohusiana na Kilimo cha Samaki.

Mamlaka husika ya Ufugaji wa Samaki itafuatilia shughuli za kilimo cha Samaki kwa miaka miwili ya kwanza na ikiwa ni ya kuridhisha, Kibali cha uendeshaji kwa muda mrefu kitatolewa.
 
Hata hivyo, leseni za uanzishwaji na uendeshaji wa Kilimo cha Samaki kwenye 
Ziwa Victoria hazitatolewa kwa zaidi ya Miaka Kumi (10) Mfululizo.

Jumatano, 15 Februari 2017

"BIOSECURITY" ina umuhimu gani kwenye shamba lako?

Click link hii ili Uifunze hapa umuhimu wa usalama wa mazingira ya kufugia samaki (Biosecurity).




 


Kutokana na kuongezeka kwa Magonjwa ya Samaki katika nchi zinazotuzunguka zikiwemo Congo, Zambia, Msumbiji, Namibia, Angola na Afrika ya kusini,  kuna umuhimu wa kuweka Mikakati ya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa yasiyo na Mipaka kaingia na kuleta madhara. Maelezo haya yametolewa na Dr. Hamis Nikuli Mtaalamu wa Afya na tiba kwa Viumbe wanaofugwa kutoka Idara ya Ukuzaji viumbe Kwenye Maji-Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.


Jumatatu, 13 Februari 2017

SEMINA JUU YA USALAMA WA MAZINGIRA YA KUFUGIA SAMAKI NA MAGONJWA YA SAMAKI




Pichani chini ni Washiriki wa Semina ya Usalama wa Mazingira ya Kufugia Samaki na Magonjwa, Zaidi ya Mameneja kumi kutoka mashamba mbalimbali ya samaki likiwemo shamba la EDEN AGRI-AQUA CO.LTD walishiriki.

Kaimu Katibu Mkuu sekta ya Uvuvi Dr. Erasto Mosha alifungua Semina hiyo na kuwaasa washiriki kuzingatia kitakachofundishwa kwakuwa Ufugaji wa Samaki ni biashara inayolipa hapa nchini.

 

Alhamisi, 2 Februari 2017

SEMINA YA UFUGAJI SAMAKI KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI



Mnamo tarehe 27/01/2017 kampuni ya ROFACOL CO. LTD inayojihusisha na masuala ya ufugaji samaki Ukanda wa Nyanda za Juu Kusini yenye ofisi zake Kyela Mjini iliandaa semina juu ya Ufugaji Samaki. Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Kyela, ndiye alikuwa mgeni rasmi na Mfunguzi wa semina hiyo.

Katika semina hiyo watu 130 walihudhuria kutoka katika Mikoa yote iliyoko Ukanda wa Nyanda za Juu Kusini na kulikuwa na watoa mada wanne (4) ambao waliwakilisha taasisi zao, kutoka ROFACOL CO.LTD, WIZARA YA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI, TAFIRI, OFISI YA MKUU WA WILAYA KYELA. Vilevile walikuwepo wawakilishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mbeya,Ofisi ya Uhamiaji, na Afisa Mtendaji Kyela.

Dhumuni.
1. Dhumuni kubwa la semina hiyo lilikuwa kutoa elimu juu ya ufugaji samaki kwenye mabwawa na vizimba,
2. Kuhamasisha na kutoa elimu juu ya sera za ukuzaji viumbe kwenye maji
3. Kutoa elimu juu ya aina ya samaki wanaofaa kufugwa katika maeneo wanayopatikana.

Maazimio.

Maazimio sita yaliyofikiwa katika semina hiyo kama ifuatavyo:- 


  1. Taratibu zote za uanzishwaji wa shughuli za ufugaji samaki na utengenezaji wa chakula cha samaki kibiashara zifuatwe, kulingana na Sera na Kanuni za Uvuvi zinavyo elekeza. 
  2. Serikali imeshauriwa kuweka kipaumbele cha kuongeza idadi ya wataalam wa ufugaji wa samaki hasa katika ngazi za chini ili wawe karibu na wafugaji wa samaki. 
  3. Taarifa ya takwimu za mabwawa na vizimba ukanda wa nyanda za juu kusini zitolewe kwenye mamlaka husika ili kuwezesha upatikanaji wake zinapohitajika. 
  4.  Uwekaji na utunzaji wa kumbukumbu kwa kila mfugaji wa samaki ulitajwa kama changamoto katika maendeleo ya ufugaji wa samaki. 
  5. Kwa kuzingatia umuhimu uliyo onekana katika semina hiyo, maazimio yalitolewa kwamba kila baada ya miezi mitatu (3) semina kama hiyo ifanyike katika kanda nyingine.