Ufugaji wa samaki
Ufugaji samaki ni kazi ya kupanda, kukuza na kutunza
samaki katika mabwawa au uzio (uliotengenezwa kwa vyuma, nyavu
au miti) au eneo lolote ambalo udhibiti wake yako chini ya mamlaka ya mfugaji mwenyewe. Mabwawa yaweza kuwa ni ya
kuchimbwa na watu (japokuwa ya asili pia huweza kutumika) wakati uzo inaweza ikawa imewekwa katika eneo lolote
lililo na maji kama ziwa na hata bahari.
au miti) au eneo lolote ambalo udhibiti wake yako chini ya mamlaka ya mfugaji mwenyewe. Mabwawa yaweza kuwa ni ya
kuchimbwa na watu (japokuwa ya asili pia huweza kutumika) wakati uzo inaweza ikawa imewekwa katika eneo lolote
lililo na maji kama ziwa na hata bahari.
Ufugaji samaki kwa
kiasi fulani si sawa na ukuaji samaki katika mito, maziwa na bahari. Tofauti
iko katika huduma inayotolewa kwa samaki wafugwao na idadi ya samaki wanaopaswa
kuwamo ndani ya eneo husika. Samaki waliofugwa huhitaji kulishwa na kuhudumiwa.
Ufugaji wa samaki si kitu kipya kabisa hapa Tanzania.
Baadhi ya Watanzania wamekuwa wakifuga samaki katika mabwawa
hata kabla ya nchi yetu kupata uhuru. Lakini baadhi ya wafugaji wamekuwa wakitoa matunzo hafifu kiasi cha kufanya
mavuno kutokuwa mazuri. Kwa miaka ya karibuni, serikali imetilia mkazo utoaji elimu (ugani) wa ufugaji samaki ili
kuboresha mafanikio yake. Kuchapishwa kwa kitabu hiki kitasaidia kuongeza uelewa wa wakulima wafugaji wa
samaki katika shughuli nzima ya ufugaji samaki nchini.
hata kabla ya nchi yetu kupata uhuru. Lakini baadhi ya wafugaji wamekuwa wakitoa matunzo hafifu kiasi cha kufanya
mavuno kutokuwa mazuri. Kwa miaka ya karibuni, serikali imetilia mkazo utoaji elimu (ugani) wa ufugaji samaki ili
kuboresha mafanikio yake. Kuchapishwa kwa kitabu hiki kitasaidia kuongeza uelewa wa wakulima wafugaji wa
samaki katika shughuli nzima ya ufugaji samaki nchini.
Faida za ufugaji samaki
Ufugaji samaki una faida nyingi sana, baadhi ni haya:
1. Chakula bora
chenye uto-mwili (protini) muhimu inayohitajika kujenga mwili.
2. Kujipatia
kipato baada ya kuuza samaki waliofugwa.
3.
Kuboresha
kazi nyingine za kilimo kama bustani ya mboga, ufugaji wa ng’ombe, bata, kuku,
nguruwe, bustani ya miti, n.k.
4. Huwezesha
kutumia rasilimali ambayo isingekuwa ikitumika kama kusingekuwa na ufugaji
samaki kama vile eneo
la ardhi lenye maji maji, pumba za mahindi na mpunga, na mabaki ya mboga mboga kutoka bustanini kwa kulishia samaki.
la ardhi lenye maji maji, pumba za mahindi na mpunga, na mabaki ya mboga mboga kutoka bustanini kwa kulishia samaki.
5. Eneo la
bwawa huwa ni sehemu nzuri ya mapumziko.
Hatua muhimu katika shughuli za ufugaji samaki
1. Uchaguzi wa
mahala panapofaa kwa ajili ya kuchimba bwawa la samaki.
2.
Tathmini ya
umbo na ukubwa wa bwawa
3.
Uchimbaji
wa bwawa.
4.
Uingizaji
na utoaji wa maji katika bwawa.
5.
Uwekaji
wa mbolea na (majivu).
6.
Upandaji
wa vifaranga vya samaki.
7.
Ulishaji
wa samaki na matunzo mengine bwawani.
8.
Uvunaji wa
samaki na aina ya nyavu/zana zifaazo kutumika.
9.
Uhifadhi wa
mbegu kwa ajili ya mzungoko mwingine wa upandaji samaki bwawani.
Joto au ubaridi wa maji katika sehemu husika huweza kuongeza au kupunguza hamu ya ulaji wa samaki na hivyo ukuaji wake.
- Chakula cha samaki (cha asili na cha ziada), aina ya chakula na kiasi kinachopatikana.
- Uwingi wa samaki waliomo bwawani kulinganisha na ukubwa wa bwawa.
- Ubora wa vifaranga (quality) waliopandwa. Vifaranga wenye ubora mruzi huwa na uwezo wa kukua haraka.
- Muda uliotumika kuzalisha samaki. Japokuwa samaki hukua haraka, wanahitaji muda wa kutosha kufikia ukubwa unaofaa kwa mahitaji ya mkulima au wa soko.
- Uwepo wa magugu na mimea isiyohitajika bwawani.
- Uwepo wa maadui wa samaki (predators).
- Kuwa na tabia ya kuvua bwawa kila baada ya miezi 6 hadi 9 kwa kulikausha ili kuboresha mazingira yake.
- Huduma inayotolewa bwawani husaidia kupatikana samaki wakubwa na wenye afya.
hakika nimefurahi sana kupata maelekezo ya namna ya kufuga samaki. nahitaji kuchimba kisima lakini maelekezo ya namna ya kuchimba kisima hayajitosherezi kwa mfano:- kisima kinajengwa na tofari baadae unakandika na udogo mfinyanzi au inakuaje, nisaidie nielewe nahitaji kuchimba leo hata kesho
JibuFutaHuwa tunaita Bwawa la kufugia samaki. Matofali na sementi vinaweza kutumika endapo udongo wa eneo unaloweka hilo bwawa una asilimia kubwa ya Mchanga, ambao hupoteza maji kwa wingi.
Futanina eneo la kutosha nahitaji msaada wa namna ya kuchimba kisima kwa ajili ya kufuga samaki aina ya perege kama nilivyosoma katika tovuti hii. naishi dar es salaam nitafarijika sana nikifunzwa namna ya kuchimba kisima kwa urefu na mapana
JibuFutaBwawa huwa linatakiwa kuwa na urefu wa wastani kati ya Mita 1.5 mpaka 1.8, upana na urefu unategemea eneo husika lina ukubwa gani...!
Futa