Jumapili, 30 Juni 2013

KUZALIANA KWA WINGI NDANI YA BWAWA NA NJIA ZA KUDHIBITI


Kuwepo kwa samaki wengi kuliko idadi inayotakiwa ndani ya bwawa (overpopulation in ponds)
  1. Kwa kawaida, samaki jamii ya perege wako katika makundi mawili kutegemeana na wanavyo tunza mayai/watoto wao wakati wa kuzaliana. Perege jamii ya Oreochromis aureus, O. mossambicus na O. niloticus hutaga kwenye viota lakini hutunza mayai/vifaranga vyao midomoni kwa ajili ya kuyalinda dhidi ya maadui.
  2. Perege wa jamii ya T. rendalli na T. zilli hutaga na kutunza mayai/vifaranga vyao kwenye viota vinavyochimbwa na dume na jike kwa pamoja. Hulinda mayai/vifaranga vyao wakiwa kwenye viota na si kuwatunza kwenye midomo mdomoni panapotokea hatari.
  3. Urahisi wa jinsi wanavyo zaliana ni moja ya sababu inayofanya perege afae kwa ajili ya kufugwa kirahisi. Lakini, tabia hii pia husababisha matatizo. Uwezekano wa kukuza vifaranga wengi ni mkubwa na husababisha kuwepo samaki wengi kwenye bwawa kuliko uwezo wa bwawa.  Matokeo yake samaki hudumaa kutokana na uhaba wa chakula, hewa na hata sehemu za mapumziko. Katika hali hii, kuna uwezekano mkubwa kukuta samaki zaidi ya asilimia 75% wakiwa na ukubwa wa chini ya uzito wa gramu 100. Kwa maeneo ambayo samaki wadogo huliwa, hili linawezekana lisiwe tatizo, lakini kama lengo ni kuuza na kujipatia fedha, samaki wa ukubwa huu huuzika kwa taabu au kwa hasara. Katika kuzuia hali hiyo ya kudumaa samaki isitokee, yafuatayo huweza kufanyika:


Njia za kuweza kudhibiti uwingi wa perege kutokea kwenye bwawa
  1. Uvunaji wa mara kwa mara wa vifaranga kwa kutumia wavu. Njia hii hufaa kwenye bwawa dogo, ina shuruba na haihitaji uzoefu ili vifaranga wasife kutokana na majeraha watakaopata wakati wa kuwavua.
  2. Kutenganisha jinsia baada ya vifaranga kuwa na ukubwa wa kuweza kutenganishwa (monosex culture
  3. Kwa kawaida, madume hukua haraka kuliko majike. Hivyo, wengi hupendelea kufuga madume
  4. Kazi ya kutenganisha huweza kufanywa na mfugaji yeyote baada ya kuonyeshwa tofauti iliyopo kati ya jinsia moja na nyinge. Mkulima anashauriwa amuone mtaalam wa uvuvi aliye karibu naye kwa maelekezo.
  5. Katika mchakato wa kuwatenganisha, makosa huweza kufanyika na kusababisha baadhi ya jinsia tofauti kutotenganishwa, mkulima asikate tamaa kwani idadi itakayokuwa imetenganishwa bado itatoa tija nzuri.
  6. Kupandikiza vifaranga machotara (stocking hybrid "all-male" fingerlings: Madume hukua haraka kuliko majike
  7. Utahitaji samaki wazazi waliohakikiwa ubora wake (requires pure strains of broodstock.
  8. Utahitaji sehemu maalum ya kuzalishia na mtaalam aliyefuzu.
  9. Ili kukidhi mahitaji ya vifaranga wa perege kwa wafugaji, kuna umuhimu wa wafugaji binafsi kuanzisha “hatcheries” kwa ajili ya kuzalisha vifaranga bora na kuwauzia wengine wenye kuhitaji. Japo kuwa kwa sasa baadhi ya wafugaji huzalisha vifaranga na kuwauzia au kuwagawia wenzi wao, wafugaji hazalisha vifaranga hao kama sehemu ya uzalishaji wa samaki wa kawaida kwenye bwawa. Kwa kadiri shughuli hii inavyokuwa, wafugaji wengi hupendelea kupata vifaranga bora. Na kwa jinsi hii, “hatchery” itakayokuwa ikizalisha vifaranga bora itapata soko zuri la vifaranga wake.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni